MIF YAHITIMISHA MAFUNZO YA SIKU TANO YA UOKAJI KWA WANAWAKE NA VIJANA
Mwanamke Initiatives Foundation (MIF) imehitimisha kwa mafanikio mafunzo ya siku tano ya uokaji yaliyolenga kuwawezesha wanawake na vijana kupata ujuzi wa vitendo utakaowasaidia kujiajiri, kuongeza kipato na kuchangia maendeleo ya kiuchumi ya jamii.